KRISTO ALIAGIZA
TUKUMBUKE ‘SIKU YA PASAKA’ AU ‘MEZA YA BWANA’? JE, ‘PASAKA’ NI ‘SIKU’? ‘PASAKA’
NI SAWA NA ‘EASTER’?
UTANGULIZI
Ni ukweli usiopingika kwamba kufa na kufufuka kwa Kristo ndilo tumaini letu. Kama Kristo hangekufa na kufufuka (kushinda kifo) imani yetu ingekuwa ni bure kabisa. 1 Kor 15:14,17-20 “tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure. Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu. Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea. Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote. Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.”
Kumbuka siku ya sabato ilianzishwa wakati wa uumbaji kabla ya anguko (dhambi). Adamu alipoanguka alituuza kwa shetani hivyo tukahukumiwa na kupotea milele. Mungu akamtuma Adamu wa mwisho ili ajaribiwe kama Adamu wa kwanza na kutununua (kutukomboa) kwa vile shetani alikuwa anatumiliki kihalali kutokana na kosa la Adamu wa kwanza. 1 Wakorintho 15:45 “Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.” Adamu wa kwanza alikuwa ni nafsi iliyo hai (living being) na Adamu wa mwisho (Yesu Kristo) akawa ni roho inayohuisha (life-giving Spirit).
Kwa vile kufufuka kwa Yesu ndiko kumerudisha thamani ya mwanadamu na uhusiano wake na Mungu, Kanisa la kwanza walianza kuabudu siku ya kwanza ya juma (siku aliyofufuka Bwana Yesu). Mdo 20:7 “Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.” 1 Kor 16:2 “Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja.”
Bwana Yesu akiwa duniani kimwili aliadhimisha Pasaka hadi Yeye mwenyewe alipofanyika Pasaka kwa ajili yetu. Hata hivyo Pasaka haikusherehekewa kama ilivyo leo bali kulikuwa na mwongozo maalum. Yohana 11:55 “Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; na wengi wakakwea toka mashambani kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka, ili wajitakase.”
UHUSIANO WA “PASAKA”, “MEZA YA BWANA” NA “KRISTO”
1.
Pasaka ilianzishwa na Mungu kwa ajili ya taifa la Israeli wakati meza ya Bwana
ilianzishwa na Kristo kwa ajili ya Wakristo.
Israeli
waliagizwa kuikumbuka SIKU HII lakini Kristo aliagiza akumbukwe YEYE MWENYEWE
kwa njia ya MEZA YA BWANA
Pasaka
ilianzishwa kwa ajili ya Waisraeli. Kut 12:12-14 “Maana nitapita kati ya
nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya
Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya
Misri; Mimi ndimi Bwana. Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba
mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu, lisiwapate pigo
lo lote likawaharibu, nitakapoipiga nchi ya Misri. Na siku hii itakuwa
ukumbusho kwenu, nanyi mtaifanya iwe sikukuu kwa Bwana; mtaifanya iwe sikukuu
katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele.”
Meza
ya Bwana ilianzishwa na Kristo kwa ajili ya Wakristo. Lk 22:19 “Akatwaa
mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, Huu ndio mwili wangu unaotolewa
kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
2.
Pasaka na Meza ya Bwana vyote vilianzishwa na Mungu ‘usiku’ kabla ya tukio la
ukombozi.
3.
Pasaka na Meza ya Bwana vyote vilihusisha mwanakondoo.
Tulinganishe
mwanakondoo (mnyama) na Mwanakondoo (Kristo)
Pasaka
ya Israeli – mwanakondoo (mnyama) Kut 12:3 “Semeni na mkutano wote wa
Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo,
kwa hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja.”
Pasaka
ya Wakristo – Mwanakondoo (Kristo) 1 Kor 5:7 “Basi, jisafisheni, mkatoe ile
chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa
maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo.”
(i).
Mwanakondoo alitakiwa kuwa mume
aliyekomaa (awe
amekomaa anayeweza kujisimamia bila kuwa tegemezi kwa mama yake)
Mwanakondoo
alitakiwa kuwa mume wa mwaka 1. Kut 12:5 “Mwana-kondoo wenu atakuwa hana
ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi.”
Kristo
ana sifa hizi za mwanakondoo.
Katika
Agano la Kale watu waliingia katika utumishi wa hema ya kukutania kati ya umri
wa miaka 30 hadi 50.
Hes
4: 2,3 “Katika wana wa Lawi uitenge hesabu ya wana wa Kohathi, kwa jamaa zao,
na nyumba za baba zao, tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi
hata umri wa miaka hamsini, wote waingiao katika utumishi huo, ili kufanya
kazi ya hema ya kukutania.”
Kristo
alianza rasmi huduma yake akiwa na miaka kama 30.
Lk
3:23 “Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama
miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli.” – Alikuwa mwanaume
mwenye umri unaotambulika kwamba amekua.
(ii).
Mwanakondoo aliangaliwa/alichunguzwa kwa takriban siku tatu.
Kut
12:3,5,6 “Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya
mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa hesabu ya nyumba ya baba zao,
mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja; Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume
wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi. Nanyi mtamweka hata
siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa
Israeli watamchinja jioni.”
Kondoo
alichunguzwa kwa siku tatu kwa sababu kuu mbili: Kwanza, kumchunguza kama ana
ila (kasoro). Pili, kumpa muda wa kujisafisha
Akigundulika
ana ila, anakuwa hafai kwa sadaka. Muda huu alinyimwa chakula ili uchafu wote
utoke afae kuokwa (kuroast) akiwa mzima.
Muda
wa Kristo tangu kuanza huduma hadi kifo chake ilipita miaka 3 na nusu. Alikufa
na kufufuka baada ya siku 3. Mathayo 12:40 “Kwani kama vile Yona alivyokuwa
siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu
atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.” Hapa tunapata
swali jingine la kujiuliza. Je ni kweli Bwana Yesu alikufa Ijumaa? Kama alikufa
Ijumaa na kufufuka baada ya siku 3 mchana na usiku, ina maana alifufuka
Jumatatu!
Maadui
walijaribu kutafuta ‘ila’ kwa Kristo bila mafanikio. Alijaribiwa na shetani
akashinda. Alikufa msalabani bila ila wala waa lolote. Akawa Mwanakondoo asiye
na ila, Pasaka wetu.
1
Petro 1:19 “bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila,
asiye na waa, yaani, ya Kristo.”
(iii).
Mwanakondoo alichinjwa jioni kuanzia saa 9 kuendelea.
Kut
12:6 “Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko
lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni.”
Sababu
ya kumchinja jioni ilikuwa ni ili kila familia iweze kumuandaa mwanakondoo
kabla ya giza kuingia.
Kristo
(Mwanakondoo wa Mungu) pia alikufa saa 9.
Mk
15:34-38 “Na saa tisa Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi,
lama sabakthani? Maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Na
baadhi yao waliosimama pale, walisema, Tazama, anamwita Eliya. Na mmoja akaenda
mbio, akajaza sifongo siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha, akisema,
Acheni, na tuone kwamba Eliya anakuja kumtelemsha. Naye Yesu akatoa sauti kuu,
akakata roho. Pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini.”
(iv).
Mwanakondoo aliliwa ndani ya nyumba bila kuvunja mfupa
Kut
12:43-46 “Bwana akawaambia Musa na Haruni, Amri ya pasaka ni hii; mtu mgeni
asimle; lakini mtumishi wa mtu awaye yote aliyenunuliwa kwa fedha, ukiisha kumtahiri,
ndipo hapo atamla pasaka. Akaaye kwenu hali ya ugeni, na mtumishi aliyeajiriwa,
wasimle pasaka. Na aliwe ndani ya nyumba moja; usiichukue nje ya nyumba nyama
yake yo yote; wala msivunje mfupa wake uwao wote.”
Kristo
(Mwanakondoo wa Mungu) alipokuwa msalabani hakuvunjwa mfupa.
Yn
19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja
miguu.”
JE PASAKA NI SAWA NA EASTER
Kutoka 20:3-5 “Usiwe na miungu mingine ila mimi. Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao.”
Easter ni tamasha la
ngono. Jina Easter ama limetokana na Ishtar, mungu wa uzazi wa
Mesopotamia, au Eostre, mungu wa kike wa Kijerumani wa majira ya
kuchipua.
Dini nyingi za kale zilifanya
ibada ya jua, au ngono.
Mayai na sungura siku ya
pasaka ni ishara za uzazi za Babeli. Kile ambacho kanisa limefanya hapo ni
kuchukua tamasha la kipagani la ngono, ambalo katika kuanzishwa kwake awali
katika ibada ya Ishtar lilihusisha kulawitiwa na makasisi wa hekalu pamoja na
matendo ya kimila ya ngono na uasherati, na kujaribu kuhusianisha na Yesu.
Jiulize, jinsi gani
Mungu anajisikia anapoona kifo na ufufuo wa Mwana wake mpendwa unahusianishwa
na ibada chafu ya kipagani ya ngono?
Ikiwa huniamini,
ninakuhimiza uangalie asili ya sikukuu hizi. Hakuna siri, ili mradi uwe na nia
ya kujifunza bila kutetea historia ya dini na mapokeo ya wanadamu.
Lazima tujiulize kwanini
siku ya Pasaka inabadilika kila mwaka. Ikiwa Kristo alifufuka Machi 10, hiyo
ingekuwa ukumbusho wa kila mwaka. Lakini niligundua kuwa tarehe ya Pasaka
inathibitishwa na unajimu (astrology according to the vernal
equinox). Sherehe ya mwanzo wa masika
(spring) ya ibada ya kipagani ya jua na majira yaliyofanywa upya iliwekwa pia
katika tarehe iyo hiyo. Iliaminika kuwa mungu astarte alianguliwa kutoka kwenye
yai kubwa lililoanguka kutoka mbinguni. Druids (waabudu shetani) huko Ulaya
walitumia mayai kama ishara za mungu wa kike wa majira ya kuchipua. Sungura
inahusishwa na mwezi katika Misri ya kale. Ni ishara ya uzazi.
Kut
23:13 “Yaangalieni hayo yote niliyowaambia; wala msitaje kabisa majina ya
miungu mingine, wala yasisikizwe kutoka kinywani mwako.”
Yos 23:7,8 “Msiingie kati ya mataifa haya, yaani, haya yaliyobaki kati yenu; wala msitaje majina ya miungu yao, wala kuwaapisha watu kwa majina hayo, wala kuitumikia, wala kujiinamisha mbele yao; bali shikamaneni na Bwana, Mungu wenu, kama mlivyotenda hata hivi leo.”
Ukisoma Catholic Encyclopedia, kanisa katoliki ndilo lilileta mabadiliko haya yote ili yaadhimishwe kwa mtindo wa "Kikristo". Fuatilia, Easter Controversy (https://www.newadvent.org/cathen/05228a.htm) Katika hatua ya pili ya mabishano ya Pasaka (Easter controversy) kwenye Baraza la Nisea (325 BK). ilikubaliwa kwamba sikukuu ya Pasaka sikuzote ilipaswa kufanywa siku ya Jumapili, na haikupaswa kuwa sanjari na awamu fulani ya mwezi, ambayo inaweza kutokea siku yoyote ya juma, mzozo mpya ulizuka kuhusu uamuzi wa Jumapili yenyewe.
Maamuzi ya Baraza
1. Lazima
Pasaka iadhimishwe na watu wote duniani kote katika Jumapili hiyohiyo moja;
2.
Jumapili hiyo lazima iwe baada ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa pasaka;
3.
Mwezi ule ulipaswa kuhesabiwa kuwa ni mwezi wa pasaka ambao siku yake ya kumi
na nne ilifuata ikwinoksi ya masika;
4. Utoaji fulani unapaswa kufanywa, pengine na Kanisa la Aleksandria lililo na ujuzi bora katika hesabu za unajimu, kwa ajili ya kuamua tarehe sahihi ya Pasaka na kuiwasilisha kwa ulimwengu wote (ona Mtakatifu Leo kwa Mfalme Marcian huko Migne, P.L., LIV, 1055).
Dr. Lawi Mshana, Freelance Facilitator & Public Speaker, Tanzania
Please send your love gift to support this ministry. +255 712924234
or CRDB Bank; Account Name: Lawi E. Mshana; Account Number: 0152219784300; Swift Code: CORUTZTZ
0 Comments
Karibu sana na ujisikie huru kushirikisha mawazo yako au kuuliza swali tujifunze pamoja (Welcome and feel free to share your thoughts or ask questions so we can learn together)