TUVUNJE MAAGANO YA SHETANI MASHULENI (WIKI LA MAOMBEZI YA UKOMBOZI KWA WANAFUNZI)
TUVUNJE MAAGANO YA SHETANI MASHULENI
(WIKI LA MAOMBEZI YA UKOMBOZI KWA WANAFUNZI)
Unajua
watoto wetu wanakaa muda mrefu mashuleni kuliko majumbani na katika nyumba za
ibada? Unajua baadhi ya mashule yamejengwa katika maeneo ambayo awali
yalikusudiwa kuwa ya matumizi mengine? Unajua hata baadhi ya walimu
wanaathiriwa na roho ya ‘backwardness and retardation’ katika maisha sababu ya
unajisi wa mashuleni? Fuatilia ujumbe huu na kushiriki katika maombi.
Tangazo
Wiki hii (Jtatu
hadi Ijumaa) hapa kanisa la TLMC (Hema) Korogwe mjini tutakuwa na maombezi
maalum ya UKOMBOZI KWA WANAFUNZI wanaoamini nguvu ya maombi. Wapo wenye
changamoto tangu walipopoteza madaftari yao au kutamkiwa kwamba hawana akili.
Maombi hayo yataambatana na ufuatiliaji wa maendeleo yao kitaaluma (kwa wale
ambao wana changamoto). Tutaombea hata madaftari yao. Wanafunzi wa shule ya
msingi watafika asubuhi na wa sekondari jioni lakini kwa KIBALI MAALUM KUTOKA
KWA WAZAZI WAO. Hasahasa kwa wale ambao hawana vipindi shuleni wakati huu wa
likizo. Kila siku itakuwa na masomo maalum ya kuombea kv Hisabati, Lugha nk.
Hakuna malipo yoyote. Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni
wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.”
Baada ya maombezi haya hatutawalaumu watoto kwa kila kitu. Tangu
nianze maombezi haya wiki hii kwa watoto wangu nimegundua kwamba changamoto zao
zingine zilipandikizwa na adui na hazisababishwi na wao wenyewe.
Piga simu hizi kwa ajili ya maelekezo: 0775-591345; 0657-528477;
0712-924234
Dr Lawi Mshana
0 Comments
Karibu sana na ujisikie huru kushirikisha mawazo yako au kuuliza swali tujifunze pamoja (Welcome and feel free to share your thoughts or ask questions so we can learn together)